Waziri Mpya wa Elimu Profesa George Magoha, ameapishwa rasmi leo kuchukua hatamu ya uongozi katika wizara hiyo. Magoha ameapishwa mbele ya Rais Uhuru Kenyatta katika halfa iliyoongozwa na Mkuu wa Utumishi wa Umma, Joseph Kinyua.
Profesa Magoha sasa ana changamoto ya kuhakikisha mtaala mpya wa elimu unaokumbwa na pingamizi unatekelezwa. Ikumbukwe alipochujwa na Kamati ya Bunge ya Uteuzi alisema ana uzoefu mkubwa katika sekta ya elimu na yu tayari kwa utendakazi.