Kalonzo na Wetangula wazuru Bungoma

Kiongozi wa Chama cha Wiper,  Kalonzo Musyoka na mwenzake wa Chama cha FORD Kenya,  Moses Wetangula wanahudhuria ibada katika Kanisa  Katoliki la Mukhweya Kabuchai Kaunti ya Bungoma ,ambapo baadaye wataongoza hafla ya mchango wa kulijenga kanisa hilo.

Viongozi hao wanatarajiwa kuangazia masuala yanayoathiri  ukuaji wa taifa hili likiwamo jinamizi la ufisadi na baa la njaa ambalo limeathiri kaunti 17 na kusababisha vifo.

Viongozi wengine wanaohudhuria ibada hiyo ni Gavana wa Bungoma Wyclifee Wangamati, Mwakilishi wa Kike, Catherine Wambilianga, Mbunge wa Kimilili, Didmus Barasa na mwenzake wa Kanduyi , Wafula wamunyinyi miongoni mwa viongozi wengine.

Kanisa hilo linahitaji takribani shilingi milioni 8 ili kukamilika.

Related Topics