Polisi wamenasa bangi baada ya gari lililokuwa likiisafirisha kupata ajali Naivasha

Gari dogo aina ya Toyota Saloon lililokuwa likisafirisha misokoto ya bangi limehusika kwenye ajali katika barabara kuu ya Nairobi Nakuru.

Watu wawili wamejeruhiwa kwenye ajali hiyo iliyofanyika karibu na Shamba la Dalemare katika Eneo la Naivasha.

Maafisa wa polisi wa Kitengo cha Trafiki waliofika kwenye eneo la tukio wamesema kwamba mtu mmoja ametoroka licha ya kuwa na majeraha mabaya.