Mwili wa msichana wapatikana umetupwa mjini Mombasa

Mwili wa msichana mwenye umri wa kati ya miaka 20 na ishirini na mitatu umepatikana umetupwa kando ya barabara kwenye eneo la Mwembelegeza Bamburi Kaunti ya Mombasa mapema leo.

Naibu Chifu wa eneo hilo, Victor Charo amesema mwili huo umepatikana na majeraha kadhaa ishara kwamba huenda msichana huyo ameuliwa.

Charo aidha amesema kwamba msichana huyo haishi katika mtaa huo hivyo huenda ameuliwa mahali kwingine na kutupwa eneo hilo.

Mwili wa msichana huyo umepelekwa katika hifadhi ya maiti katika Hospitali ya Rufaa ya Coast General ambako utafanyiwa upasuaji huku polisi wakiendeleza uchunguzi kufuatia kisa hicho.Mwili wa msichana mwenye umri wa kati ya miaka 20 na ishirini na mitatu umepatikana umetupwa kando ya barabara kwenye eneo la Mwembelegeza Bamburi Kaunti ya Mombasa mapema leo.

Naibu Chifu wa eneo hilo, Victor Charo amesema mwili huo umepatikana na majeraha kadhaa ishara kwamba huenda msichana huyo ameuliwa.

Charo aidha amesema kwamba msichana huyo haishi katika mtaa huo hivyo huenda ameuliwa mahali kwingine na kutupwa eneo hilo.

Mwili wa msichana huyo umepelekwa katika hifadhi ya maiti katika Hospitali ya Rufaa ya Coast General ambako utafanyiwa upasuaji huku polisi wakiendeleza uchunguzi kufuatia kisa hicho.

Related Topics