Mchakato wa kukusanya saini ili kuvunjwa kwa Bunge la Kaunti ya Mombasa unaendelea huku Mashirika ya Kijamii yakisema kwamba Gavana Joho hana mamlaka Kikatiba kulivunja bunge hilo.
Kulingana na mashirika hayo, gavana Joho amekuwa akiwahujumu wawakilishi wadi hasa wanapoukosoa uongozi wake. Wawakilishi wadi hao wameshauriwa kuhakikisha wanaendesha shughuli zao bila kutishwa na yeyote.