Bunge limeidinisha uteuzi wa Profesa George Magoha kuwa waziri mpya wa Elimu. Kiongozi wa wachache kwenye bunge la Kitaifa John Mbadi, amewasilisha ripoti na mapendekezo kuhusu uteuzi huo baada ya kumchuja Magoha juma lililopita.
Bunge sasa litajadili mapendekezo ya kamati hiyo kuhusu uteuzi wake kesho alasiri. Alipofika mbele ya Kamati ya Uteuzi Magoha alisema anatajriba na uzoefu wa kutosha katika nyanja ya elimu ambapo amehudumu kwa muda mrefu.
Magoha amemtaridhi Amina Mohammed ambaye amehamishiwa Wizara ya Michezo ambayo awali ilishikiliwa na Rashid Echese aliyesimamishwa kazi na Rais Uhuru Kenyatta.