Shillingi bilioni 17 ghushi zapatikana Barclays

Maafisa wa Kiktengo cha Flying Squad wamekita kambi katika Benki ya Barclays Tawi la  Queens, Jijini Nairobi, kuchunguza kupatikana kwa shilingi bilioni 17, fedha bandia zinazodaiwa zilikuwa zikipelekwa katika benki hiyo. 

Tayari washukiwa watatu ambao ni Wakenya wawili na raia mmoja wa kigeni wamekamatwa kwa kuhusishwa na fedha hizo.  

Si mara ya kwanza wa fedha bandia kupatikana nchini. Siku chache zilizopita mabilioni ya fedha vilevile zilipatikana katika nyumba inayodaiwa kumilikiwa na washukiwa saba wanaohusishwa na kisa cha kumlaghai mtu mfanyabiashara mmoja fedha kwa kujidai kuwa Rais Uhuru Kenyatta baada ya kuiga sauti yake.

Related Topics

Barclays Queensway