Gavana wa Mombasa Ali Hassan Joho amejitetea mbele ya Kamati ya Seneti iliyobuniwa kutatua mzozo wa kisiasa kati yake na wawakilishi wadi wa Bunge la Mombasa. Mzozo huo uliibuka baada ya Joho kudaiwa kuwa na mpango wa kuwabandua wawakilishi wadi suala ambalo amelikana vikali.
Joho amejitetea vikali dhidi ya madai hayo amesema kilichopo kwa sasa ni mvutano baina ya Spika wa Bunge na baadhi ya maafisa katika serikali.