Polisi Kwale wavamia kituo kinachoaminika kutoa mafunzo ya ugaidi

Polisi kwenye Eneo la Ngombeni Kaunti ya Kwale, mapema leo wamevamia  nyumba moja inayoaaminika kuwa kituo cha kutoa mafunzo kwa wafuasi wa Kundi la Kigaidi la Al Shabaab na kunasa silaha za uhalifu. Baadhi ya silaha zilizonaswa ni pamoja na panga, visu , mbolea ya kutengeza silaha,viberiti, sare za kijeshi  na vitabu vya dini.

Polisi pia wamenasa bendera  ya rangi nyeusi  na nyeuepe yenye maandishi yanayofungamana na makundi ya kigaidi ya  ISIS, Al-Shabaab na  Boko Haram .Aidha katika Operesheni hiyo, polisi wamenasa kifaa hatari kinachotumika kutenganeza vilipuzi.

OCPD wa Kwale, Tom Odero, anasema kwamba sehemu hiyo huenda hutumika kutoa mafunzo ya uhalifu .Odero  aidha amefichua kwamba maandishi katika bendera hiyo yamefasiriwa kumaansha  kwamba '' Tuko tayari kwa vita''. Hata hivyo ,hakuna  yeyote aliyenaswa katika nyumba hiyo wakati wa  msako huo.

Taifa la Kenya katika siku za hivi maajuzi limekumbwa na mashambulio ya kigaidi, la hivi punde likiwa shambulio la Dusit D2 la Tarehe 15 Januari, ambapo watu 21 walifariki dunia huku wengine wakijeruhiwa.

Related Topics