Rais Uhuru Kenyatta leo anatarajiwa kufungua rasmi Kongamano la Ugatuzi liliong'oa nanga mapema jana katika Chuo Kikuu cha Kirinyaga.

Rais Uhuru Kenyatta leo anatarajiwa kufungua rasmi Kongamano la Ugatuzi liliong'oa nanga mapema jana katika Chuo Kikuu cha Kirinyaga.

Kongamano hilo linatarajiwa kuangazia hatua zilizopigwa na kaunti mbalimbali katika kuwainisha ajenda zake na ajenda nne kuu za serikali ya Jubilee kufuatia mjadala ulioanza katika Kongamano la Ugatuzi mwaka uliopita kwenye Kaunti ya Kakamega. Kauli mbiu ya kongamano la mwaka huu kwa kiingereza ni Deliver, Transform, Measure, and Remain Accountable.

Jana, magavana wote walikutana na Rais Uhuru Kenyatta katika Ikulu ya Sagana, kabla ya magavana, maseneta, wawakilishi wadi na wajumbe wengine  kushiriki mashindano  ya soka.

Hayo yakijiri, wajumbe wanaohuhudhuria kongamano hilo wamelalamikia mpangilio duni  baada ya kubainika kwamba baadhi ya vibali vya kuhudhuria kongamano havikuwa vimvchapishwa licha ya kila anayehuduria kulipa shilingi elfu 20. Kadhalika, wengi wao wamelazimika kutafuta malazi katika kaunti jirani za Murang'a, Embu, Nyeri na hata mjini Thika baada ya vyumba vya malazi, Kirinyaga kujaa. 

Hali ya usalama nayo imetiliwa shaka baada ya wanahabari wa Shirika la Royal Media kupokonywa vifaa kadhaa vikiwamo vipakatalishi na kipaza sauti.

Mwenyeji wa kongamano hilo, Anne Waiguru amekiri kuwa nii vigumu kwa Kirinyaga pekee kumudu mahitaji ya watu elfu 6 watakokuwa wakihuhuria vikao hivyo hadi Ijumaa. Ikumbukwe awali, taarifa kwamba mipira ya kupanga uzazi zaidi ya elfu 150 ilikuwa imesambazwa ilizua mjadala mkali kuhusu lengo halisi la wanaohudhuria kongamano hilo.

Related Topics

ugatuzi Uhuru