Huenda wakulima wa miwa katika sehemu mbali nchini, wakapata afueni baada ya Serikali ya Kitaifa kuweka mikakati kwa ushirikiano na Viongozi mbalimbali ili kukabili changamoto zinazoikumba Sekta ya Sukari.
Katika kikao kilichoongozwa na Kinara wa ODM Raila Odinga, kwenye ofisi za Capital Hill, Odinga amesema kwamba viongozi wameafikiana kuwashirikisha washikadau wote kuimarisha kilimo cha miwa ili kutatua masaibu ya wakulima.
Waziri wa Kilimo mwangi Kiunjuri kwa upande wake amesema kwamba Sekta ya Sukari inakumbwa na changamoto si haba ,akisema wakulima wanataabika kutokana na kunyanyaswa na viwanda vya kutengeneza sukari
Mkutano huo unajiri wakati ambapo sekta ya sukari inakabiliwa na matatizo tele huku wakulima wa miwa kwenye maeneo mbalimbali wakizidai kampuni za sukari malimbikizi ya madeni yao. Aidha suala la ufisadi kwenye usimamizi wa viwanda hivyo umetajwa kuwa kizingiti kwenye ukuaji wa kilicho cha miwa.