Viongozi wa eneo la Baringo wakiongozwa na Gavana Stanely Kiptis na Mbunge wa Baringo Kusini Charles Kamuren wametoa wito kwa Tume ya Uchaguzi, IEBC kuharakisha tatizo la mpaka linatatuliwa kwenye kaunti hiyo.
Wamesema mzozo huo ndio unasababisha mivutano baina ya jamii mbalimbali hali ambayo imechangia watu kadhaa kuuliwa na wala sio wizi wa mifugo inavyoaminika.