Watu 4 wafariki dunia kufuatia ajali, Nakuru

Watu wanne wamefariki dunia kufuatia ajali kwenye eneo la Morendat Barabara kuu ya Nakuru-Nairobi mapema leo.

Afisa msimamizi wa trafiki eneo la Bonde la Ufa Ziro Arome, amesema ajali hiyo imehusisha gari la binafsi na basi ya kubeba abiria la kampuni ya   Climax.

Waliojeruhiwa wanatibiwa katika hospitali ya Naivasha.