Mwili wa mwanafunzi wapatikana katika chumba cha kukodi, Narok

 

Polisi kwenye Kaunti ya Narok wanafanya uchunguzi kufuatia kisa ambapo mwili wa mwanafunzi wa kidato cha tatu umepatikana katika chumba kimoja cha kukodi. Chifu wa eneo hilo, Titus Tonui amesema mwanafunzi huyo ametambuliwa kuwa wa Shule ya Upili ya Kisiara. Tonui amesema imebainika kuwa mwanafunzi huyo alikuwa mjamzito na huenda alifariki dunia alipokuwa akijaribu kuavya mimba.

Mwanamume anayeshukiwa kuwa mpenzi wa mwanafunzi huyo anayeishi karibu na chumba hicho cha kukodi hajulikani aliko tangu kutokea kwa kisa hicho. Ikumbukwe mwaka uliopita Kamishna wa Kaunti ya Narok, George Natembeya alipendekeza kukaguliwa kwa wanafunzi wa kike kubainisha iwapo walikuwa wajawazito ama walikuwa wamekeketwa.

Hata hivyo mashirika mbalimbali ya kutetea haki za binadamu yaliupinga mpango huo yakisema unakiuka haki za wanafunzi hao na huenda ungesababisha unyanyapaa hasa kwa wale ambao wangengunduliwa kuwa wajawazito vilevile waliokeketwa.