NTSA imefutilia mbali leseni ya magari ya Green Line kufuatia ajali

Mamlaka ya Usalama Barabarani NTSA imefutilia mbali lesini ya magari ya Kampuni ya Green Line kufuatia ajali ya barabarani Jumapili, iliyosababisha vifo vya watu kumi na mmoja.

Katika taarifa kwa vyombo vya habari NTSA imesema hatua hiyo inafuatia baada ya kubainika kuwa magari hayo yalikuwa yakikiuka sheria za trafiki.

Aidha NTSA imewaagiza maafisa wa trafiki kuyakamata magari yote ya kampuni hiyo yatakayoatikana yakiendelea na shughuli zao za kawaida.

Ikumbukwe baada ya ajali hiyo baadhi ya manusura walidai kuwa dereva wa gari walilokuwa wakisafiria alikuwa akiliendesha kwa mwendo wa kasi na kupuuza malalamiko yao.