Tangu kuzinduliwa kwa mitandao ya kijamii, mitandao hiyo imetumiwa kuwa njia ya kushirikiana, na hata kuleta mabadiliko. Katika mtandao wa Twitter, Wakenya wanao utumia mtandao huo maarufu KOT, Kenyans On Twitter, wamesifika sana kwa kuhakikisha sifa za taifa hili haziharibiwi vilevile kugakikisha mashujaa wanapokea heshima wanayo stahili.
Wiki iliyopita Wakenya hao walihakikisha gazeti la New York Times linaomba radhi na kuondoa picha walizochapisha za watu walioaga dunia wakati wa shambulio katika hoteli ya DUSIT D2 bila kuficha sura zao.