Mswada wa kumbandua Waziri Sicily Kariuki wawasilishwa bungeni

Mswada unaopendekeza kuondolewa ofisini kwa Waziri wa Afya, Sicily Kariuki umewasilishwa bungeni. Jumla ya wabunge mia sabini wametia saini mswada huo uliowasilishwa na Mbunge, Bashir Abdullaih.

 Waziri huyo analengwa kutimuliwa kwa kumsimamisha kazi Afisa Mkuu Mtendaji wa Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta, KNH Lily Koros kufuatia kisa ambapo mgonjwa asiyestahili alifanyiwa upasuaji wa ubongo. Waziri huyo anashtumiwa kwa madai ya kukiuka sheria katika kufanya uamuzi huo.

Kulingana na katiba, saini za thuluthi moja ya wabunge ambao ni 116  miongoni mwa 349 zinahitajika ili kuwasilishwa kwa mswada wa kutokuwa na imani na mtu fulani. K

Hapo jana Kamati ya Bunge ya Afya iliyoandaa uchunguzi kuhusu kisa hicho ilipendekeza kubuniwa upya kwa bodi ya KNH vilevile kufanywa kwa mabadiliko ya usimamizi ya hospitali hiyo. 

Related Topics

Sicily Koros