Rosa Agutu
" Serikali ya Jubilee imelipa kipaumbele suala la elimu kwa wanafunzi na kutimiza ahadi ilizotoa kwa Wakenya''. Kauli hiyo imetolewa na Rais Uhuru Kenyatta alipowahutubia wakazi wa eneo la Eastlands, kabla ya kuelekea katika ukumbi wa KICC kuwasilisha stakabadhi zake za uteuzi pamoja na Naibu wake William Ruto. Rosa Agutu na taarifa zaidi.
Awali akihutubu katika mtaa wa Dolnholm, Rais Kenyatta amesisitiza kuwa serikali yake imejitahidi kutimiza miradi mbalimbali ya maendeleo, na kusema wanaopinga juhudi hizo hawana nia njema kwa taifa hili.