Na Sofia Chinyezi
NAIROBI, KENYA, Mlinzi wa boma la mamaye mhubiri Pius Muiru, anazuiliwa baada ya kukiri kumuua mwanamke huyo. Maafisa wa upelelezi waliupata mwili wa Cecilia Wangari Mwangi siku moja baada ya kuripotiwa kutoweka, ukiwa umezikwa katika kaburi moja nyumbani kwake eneo la Murang'a. Mshukiwa ndiye aliyewaelekeza maafisa hao hadi eneo alikomzika.
Kamanda wa Polisi Kaunti ya Murang'a, Naomi Ichami anasema mlinzi huyo na mkaza-mwana wa Wangari wanazuiliwa, na kwamba wote watakaotajwa vilevile watahojiwa.