Na Rosa Agutu
NAIROBI, KENYA, Rabsha zimeshuhudiwa katika mkutano wa Jubilee uliokuwa ukiendalia katika Ukumbi wa Bomas, Kaunti ya Nairobi kufuatia mvutano kati ya wafuasi wa Seneta wa Nairobi, Mike Sonko na wa Mbunge wa Starehe Maina Kamanda, kuhusu usimamizi wa bodi ya uchaguzi wa Kaunti ya Nairobi.
Wafuasi wa Sonko waliondoka kwenye mkutano huo ghafla wakidai kuwa Kamanda alikuwa na njama ya kuiba kura hizo kwa kumpendelea Mbunge wa Gatanga, Peter Kenneth madai ambayo yanapingwa na Kamanda.