Safari za ndege Nairobi - Mogadishu kurejelewa

 
Na Mate Tongola

NAIROBI, KENYA, Mataifa ya Kenya na Somalia yameafikiana kurejelea safari za moja kwa moja za ndege kati ya Nairobi na Mogadishu pamoja na kufunguliwa kwa vituo viwili ambavyo vitatumiwa na wanaoingia na kutoka mataifa haya mawili.

Rais Uhuru Kenyatta ametoa tangazo hili baada ya mkutano kati yake na mwezake wa Somalia, Mohammed Abdulahi Farmajo ambaye yuko nchini kwa ziara ya siku tatu, ikiwa ni ziara yake ya kwanza nje ya taifa hilo jirani tangu kuapishwa kuwa Rais.

Kwa upande wake, Farmajo ameeleza kuridhishwa kwake na kujitolea kwa Kenya kuisaidia Somalia kurejelea hali ya uthabiti kufuatia vita vya kikoo ambavyo vimedumu kwa zaidi ya miongo miwili sasa, vilevile hujuma za kundi gaidi la Al Shaabab.

Related Topics

Somalia Kenya