To Save the Planet

Ni rasmi sasa koti tamba ya Emuhaya/Luanda imezinduliwa ili kwa kutoa huduma kwa wakazi wa eneo hilo kuanzia wiki ijayo pasi na kusafiri mwendo mrefu kufika mahakama ya Vihiga na Maseno mtawalia na la mno kuashiria kupunguza idadi za kesi zinazorundika kwenye koti hizo pasi na kushughulikiwa.

 

 

Akizindua koti hiyo tamba eneo la Mulukhoro eneo bunge la Luanda, hakimu mkuu wa mahakama ya Kakameka na Vihiga kwa mpigo Bi. Ruth Sitati amedokeza kuwa nia na lengo haswa ya kufanya hivyo imetokana na kufurika kwa kesi ambazo hutoka katika kituo cha polisi cha Luanda na pia mwendo wa kusafiri maeneo ya koti za maseno na Vihiga umekuwa na ati ati swala linalosababisha utendakazi kuwa na utatanishi.

 

 

Aidha, amedokeza kuwa kupitia kamati teule ya haki kila mteja ama au mkenya yeyote yule ana haki ya kupata haki ya kuhudumiwa karibu na maeneo yao, ambapo wanazidi kuzindua koti hizo tamba maeneo mengine katika mkoa wa magharibi mwa kenya.