×
App Icon
The Standard e-Paper
Home To Bold Columnists
★★★★ - on Play Store
Read on the App

Mikakati zaidi yawekwa kuzuia udanganyifu kwenye mitihani

Na Beatrice Maganga

Serikali imezibadili saa za kufunguliwa kwa kontena zinazohifadhi karatasi za Mtihani wa Kitaifa wa Kidato cha Nne KCSE kutoka saa kumi na moja asubuhi hadi saa kumi na mbili unusu asubuhi. Wizara ya Elimu kwa Ushirikiano na Baraza la Kitaifa la Mitihani nchini KNEC wametoa muongozo huo baada ya kubainika kwamba baadhi ya walimu wakuu wamekuwa wakijaribu kufanikisha udanganyifu katika mitihani hiyo kufuatia kukabidhiwa karatasi hizo mapema.
Kwenye taarifa kupitia wa Katibu wa Wizara hiyo Belio Kipsang, walimu na wasimamizi wa mitihani aidha wameonywa dhidi ya kuzungumzia masuala ya mitihani hiyo kwenye mitandao ya kijamii ili kuzuia kuhujumu kufanyika kwa mitihani hiyo kwa njia inayostahili.
Amesema Mwenyekiti wa KNEC George Magoha ndiye pekee aliye na mamlaka ya kuwasilisha taarifa kuihusu mitihani inayoendelea.

 

Get Full Access for Ksh299/Week
Bold Reporting Takes Time, Courage and Investment. Stand With Us.
  • Unlimited access to all premium content
  • Uninterrupted ad-free browsing experience
  • Mobile-optimized reading experience
  • Weekly Newsletters
  • MPesa, Airtel Money and Cards accepted
Already a subscriber? Log in