Please enable JavaScript to view advertisements.
×
App Icon
The Standard e-Paper
Home To Bold Columnists
★★★★ - on Play Store
Download App

Kenya Airways yasema abiria waliokuwa kwenye ndege iliyopatwa na hitilafu wako salama

Na Beatrice Maganga

Shirika la Ndege la Kenya Airways, limesema abiria waliokuwa wakisafiria mojawapo ya ndege zake iliyokumbwa na matatizo ikiwa angani wako salama. Kwenye taarifa, shirika hilo limesema kwa sasa ndege hiyo iliyokuwa ikisafiri kutoka Uganda Jumatatu jioni inakaguliwa na wahandisi. Mojawapo la magurudumu ya ndege hilo lilipasuka ilipokuwa ikitua katika uwanja wa JKIA.
Katika siku za hivi karibuni, misururu ya visa kuhusu hitilafu za ndege imeshuhudiwa nchini. Wiki iliyopita ndege moja ilianguka katika Msitu wa Kibiku Ngong ambapo rubani na mwanafunzi wake walijeruhiwa. Siku chache zilizopita ndege nyingine ya polisi ilianguka katika Mtaa wa Mathare na kuwajeruhi polisi wanne.
Mtalii mmoja aidha alifariki dunia wakati ndege aliyokuwa ameabiri na wenzake kuanguka eneo la Naivasha. Wengine walijeruhiwa wakati wa kisa hicho.
 

 

Premium Article

Get Full Access for Ksh299/Week.

Bold Reporting Takes Time, Courage and Investment. Stand With Us.
Continue Reading  →
What you get
  • Unlimited access to all premium content
  • Ad-free browsing experience
  • Mobile-optimised reading
  • Weekly newsletters & digests
Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payments Kenya's most trusted newsroom since 1902
Support Independent Journalism

Stand With Bold Journalism.
Stand With The Standard.

Journalism can't be free because the truth demands investment. At The Standard, we invest time, courage and skills to bring you accurate, factual and impactful stories. Subscribe today and stand with us in the pursuit of credible journalism.

Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payment Kenya's most trusted newsroom since 1902

Follow The Standard on Google News