Na, Sophia Chinyezi
Benki za humu nchini zimepoteza katika jitihada zao za kuzuia kudhibitiwa kwa viwango vya riba vinavyotozwa wanaochukua mikopo, baada ya Rais Uhuru Kenyatta kusaini kuwa sheria Mswada wa Marekebisho wa Benki wa mwaka 2015. Hatua hiyo inazizuia benki kuongeza riba zinazotozwa mikopo kuwa zaidi ya asilimia nne ya riba iliyoratibiwa na Benki Kuu. Huku Benki Kuu ikiwa katika asilimia 10.5, benki sasa haziwezi kutoza riba ya zaidi ya asilimia 14.5 kwa mikopo.