×
App Icon
The Standard e-Paper
Kenya’s Boldest Voice
★★★★ - on Play Store
Download App

Olo Mide Afungwa Jela

Na, Beatrice Maganga

Mwanamuziki maarufu wa Rhumba, Koffi Olomide amehukumiwa kifungo cha miezi kumi na minane gerezani jijini Kinshasa, katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.
Mahakama ya Kinshasa vilevile imemnyima Olomide fursa ya kulipa dhamana ya pesa taslimu badala ya kuhudumu kifungo hicho kwa kumpiga teke mcheza-densi wake wa kike uwanjaji JKIA, Nairobi, Ijumaa iliyopita.
Koffi alikamatwa mapema leo nyumbani kwake jijini Kinshasa kufuatia agizo lililotolewa na Mwendesha Mashtaka wa DR Kongo. Awali mmoja wa raia wa nchi hiyo, Zakarie Bababaswe aliwasilisha kesi mahakamani akitaka mwanamuziki huyo akamatwe kwa kumdhulumu mwanadada huyo.
Olomide alirejeshwa nchini mwake kufuatia kisa cha kumdhulumu mwanabendi huyo, kisa kilichochea hisia kali ndani na nje ya nchi. Aidha alizuiwa kuwatumbuiza mashabiki wake katika ukumbi wa Bomas Nairobi, vilevile nchini Zambia.

 

Get Full Access for Ksh299/Week.
Fact‑first reporting that puts you at the heart of the newsroom. Subscribe for full access.
  • Unlimited access to all premium content
  • Uninterrupted ad-free browsing experience
  • Mobile-optimized reading experience
  • Weekly Newsletters
  • MPesa, Airtel Money and Cards accepted
Already a subscriber? Log in