The Standard Group Plc is a
multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper
print operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The
Standard Group is recognized as a leading multi-media house in Kenya with a key
influence in matters of national and international interest.
Familia sita zimeachwa bila makao kwenye Kaunti ya Narok baada ya watu wasiojulikana kuteketeza nyumba zao usiku wa kuamkia Jumanne. Takribani nyumba kumi zimeteketezwa wakati wa kisa hicho kilichotokea kwenye maeneo ya Pimbiniet na Olopirik mpakani pa Transmara Mashariki na Magharibi, mwendo wa saa tatu usiku na saa tano.
Inaarifiwa kisa hicho kilitokea kufuatia tofauti zilizoibuka kati ya jamii za Kipsigis na Maasai. Kwa mujibu wa wa OCPD wa Transmara, Ambrose Hongo, kisa hicho kilijiri wakati wenyeji walipokuwa wamelala na kusema maafisa wa usalama wanafanya uchunguzi kuwatambua wahusika.
Hata hivyo amesema kufikia sasa, hakuna aliyekamatwa akihusishwa na kisa hicho, ingawa polisi wameimarisha doria kwenye mpaka unaozitenganisha jamii hizo. Kisa hicho kinajiri wiki kadhaa baada ya kamati ya usalama eneo hilo kuwaonya wakazi dhidi ya kumiliki silaha hatari.
Premium Article
Get Full Access for Ksh299/Week.
Fact-first reporting that puts you at the heart of the newsroom. Subscribe for full access.
🔥 Flash Sale !
Subscribe now and enjoy 50% off monthly and annual plans. Offer ends in…
Stand With Bold Journalism.
Stand With The Standard.
Journalism can't be free because the truth demands investment.
At The Standard, we invest time, courage and skills to bring you accurate,
factual and impactful stories. Subscribe today and stand with us in the
pursuit of credible journalism.