Mpeperusha bendera wa Muungano wa Azimio Raila Odinga sasa anadai kuwa hatashiriki katika mjadala wa Kitaifa wa wawaniaji wa urais na mshindani wake, William Ruto wa UDA.
Msemaji wa kamati ya Kampeni ya Raila Profesa Makau Mutua anadai kuwa mfumo wa mjadala wa marais nchini ambapo washindani wa karibu wanawekwa pamoja kuulizwa maswali si mzuri.
Katika taarifa kwa vyombo vya Habari profes Mutua amedai kuwa mjadala huo wa wagombea wa urais pia haulengi kujadili masuala ya uongozi, ufisadi na maadili ambayo ndiyo yanawahusu moja kwa moja Wakenya.