Please enable JavaScript to view advertisements.
×
App Icon
The Standard e-Paper
Smart Minds Choose Us
★★★★ - on Play Store
Download App

Rais asema hakuona umuhimu wa kuhudhuria mjadala wa urais

Na, Beatrice Maganga/ John Mbuthia
Rais asema hakuona umuhimu wa kuhudhuria mjadala wa urais
Siku moja baada ya kukosa kuhudhuria mjadala wa urais, Rais Uhuru Kenyatta leo hii ameendeleza kampeni kwenye Kaunti za Murang'a na Nyeri huku akichukua fursa hiyo kufafanua sababu za kutohudhuria mjadala huo. John Mbuthia ameifuatilia ziara hiyo ya Rais na hii hpa taarifa yake.
Akihutubu katika eneo la Mukurweni ambalo hakulizuru awali wakati wa ziara yake siku chache zilizopita, Rais Kenyatta amesema alikosa kuhudhuria mjadala kwa kuwa haukona haja ya kufanya hivyo akisema maendeleo aliyowafanyia wananchi yako bayana
Uhuru ambaye amesema alimtazama Raila katika runinga wakati wa mjadala huo, amemshtumu kwa kusema hakuwa na mamlaka ya moja kwa moja ya kukabili ufisadi alipokuwa katika serikali ya mseto.
Rais Kenyatta aidha hakukosa kuvishtumu vyombo vya habari akisema havijakuwa vikimuunga mkono tangu uchaguzi mkuu wa mwaka 2013.Rais Kenyatta ameendeza ziara maeneo ya Tetu  na kuwaahidi wakazi kwamba atabuni kata mpya eneo hilo.
Katika Eneo Bunge la Othaya, Rais ameahidi kufunguliwa kwa hospitali ya Rufaa ya Othaya Februari mwaka ujao huku huduma za akina mama kujifungua bila malipo zikiendelea kuboreshwa.  
Naibu wa Rais, William Ruto ambaye ameendeleza kampeni kwenye kaunti za Vihiga na Kakamega kwa upande wake ameyakosoa madai ya Raila kuwa kuna njama ya kuwahusisha maafisa wa usalama katika kufanikisha udanganyifu wakati wa uchaguzi mkuu.

Premium Article

Get Full Access for Ksh299/Week.

Uncover the stories others won't tell. Subscribe now for exclusive access.
Continue Reading  →
What you get
  • Unlimited access to all premium content
  • Ad-free browsing experience
  • Mobile-optimised reading
  • Weekly newsletters & digests
Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payments Kenya's most trusted newsroom since 1902
Support Independent Journalism

Stand With Bold Journalism.
Stand With The Standard.

Journalism can't be free because the truth demands investment. At The Standard, we invest time, courage and skills to bring you accurate, factual and impactful stories. Subscribe today and stand with us in the pursuit of credible journalism.

Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payment Kenya's most trusted newsroom since 1902

Follow The Standard on Google News

Related Topics