Please enable JavaScript to view advertisements.
×
App Icon
The Standard e-Paper
Join Thousands Daily
★★★★ - on Play Store
Download App

Rais akabidhiwa ripoti kuhusu ukame

Na Sophia Chinyezi
Rais Uhuru Kenyatta amekabidhiwa ripoti kuhusu hali ya ukame nchini na mikakati iliyowekwa na serikali kuu na washikadau wengine kukabili hali. Mawaziri na makatibu wa Wizara za Ugatuzi, Fedha, Kilimo, Leba na Masuala ya Afrika Mashariki, wamemueleza Rais kwamba kaunti ishirini na tatu zilizo katika maeneo ya jangwani zimeathirika pakubwa na ukame.
Hata hivyo wamesema mikakati mwafaka imewekwa kuhakikisha hakuna Mkenya atakakufa kutokana na njaa. Rais Kenyatta amesema atakutana na mawaziri hao tarehe 27 mwezi huu kupata ripoti kamili ya hali hiyo. Aidha ameongeza kuwa watatathmini bajeti kushughulikia tatizo hilo, huku akiziomba serikali za kaunti kubuni mikakati itakayosaidia kupata suluhu ya ukame.
Waziri wa Fedha Henry Rotich na mwenzake wa Ugatuzi Mwangi Kiunjuri wamemfahamisha Rais kuhusu uamuzi wao wa kuwashirikisha washikadau wengine ambao wako katika maeneo yaliyoathirika ili kutoa usaidizi unaohitajika.
Mawaziri hao vilevile wamesema serikali imekuwa ikisambaza chakula cha msaada kwa Wakenya milioni 1.5, wengi wakiwa wa maeneo ya jangwani.

Premium Article

Get Full Access for Ksh299/Week.

Bold Reporting Takes Time, Courage and Investment. Stand With Us.
Continue Reading  →
What you get
  • Unlimited access to all premium content
  • Ad-free browsing experience
  • Mobile-optimised reading
  • Weekly newsletters & digests
Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payments Kenya's most trusted newsroom since 1902
Support Independent Journalism

Stand With Bold Journalism.
Stand With The Standard.

Journalism can't be free because the truth demands investment. At The Standard, we invest time, courage and skills to bring you accurate, factual and impactful stories. Subscribe today and stand with us in the pursuit of credible journalism.

Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payment Kenya's most trusted newsroom since 1902