Please enable JavaScript to view advertisements.
×
App Icon
The Standard e-Paper
Kenya’s Boldest Voice
★★★★ - on Play Store
Download App

Maafisa wakuu katika Wizara ya Afya watakiwa kujiuzulu kufuatia sakata ya shilingi bilioni tano

Na Carren Omae

Sakata nyingine kubwa kuhusu ufujaji wa pesa katika Wizara ya Afya ambayo imeibuka tayari imechochea hisia kali nchini. Huku uchunguzi kuhusu sakata hiyo ukiendelea, baadhi ya viongozi wametoa wito kwa maafisa wakuu katika wizara hiyo kujiuzulu ili kutoa nafasi ya uchunguzi huo kufanywa.
Alhamisi Waziri wa Afya Cleopa Mailu na Katibu wa Wizara hiyo, Nicholous Muragori walikosa kufika mbele ya Kamati ya Afya ya Seneti kujibu maswali yanayohusu sakata hiyo. Sababu walizotoa ni kwamba walikuwa katika mkutano mwingine kuhusu tatizo lilo hilo, vilevile kukusanya stakabadhi watakazoziwasilisha mbele ya kamati. Mwenyekiti wa kamati hiyo Wilfred Machage ameeleza kusikitishwa na hulka za maafisa wa umma kufuja fedha zinazotengewa miradi muhimu nchini.
Baadhi ya wanachama wa kamati hiyo wamesema maafisa hao pamoja na wengine wanaohusishwa wanafaa kuwajibika. Wanakamati hao akiwamo Seneta wa Wajir, Ahmed Abdulahi na Seneta Maalumu, Ziporah Kitony wamesema wanafaa kujiuzulu nyadhifa zao.
Mailu na Muragori wametakiwa kufika mbele ya kamati hiyo Jumanne wiki ijayo.
Sakata hiyo inayoashiria kupotea kwa zaidi ya shiingi bilioni tano, inadaiwa kuwahusisha maafisa wakuu wa Wizara ya Afya waliovuruga mfumo wa ki-dijitali wa malipo ya serikali, maarufu IFMIS na kutumiwa vibaya kwa mabilioni ya pesa zilizonuiwa kununua vifaa na kulipia huduma za matibabu.  

Premium Article

Get Full Access for Ksh299/Week.

Uncover the stories others won't tell. Subscribe now for exclusive access.
Continue Reading  →
What you get
  • Unlimited access to all premium content
  • Ad-free browsing experience
  • Mobile-optimised reading
  • Weekly newsletters & digests
Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payments Kenya's most trusted newsroom since 1902
Support Independent Journalism

Stand With Bold Journalism.
Stand With The Standard.

Journalism can't be free because the truth demands investment. At The Standard, we invest time, courage and skills to bring you accurate, factual and impactful stories. Subscribe today and stand with us in the pursuit of credible journalism.

Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payment Kenya's most trusted newsroom since 1902

Follow The Standard on Google News