Please enable JavaScript to view advertisements.
×
App Icon
The Standard e-Paper
Home To Bold Columnists
★★★★ - on Play Store
Download App

Jaji Mbogholi ashindwa kuwatambua Magavana

Na, Beatrice Maganga/Mate Tongola

Shughuli ya kuwachuja wanaowania wadhifa wa Jaji Mkuu, imeingia siku ya pili leo hii huku Jaji Msagha Mbogholi akitathminiwa ili kujua iwapo anawafahamu baadhi ya viongozi wa kaunti. Mbogholi alitakiwa kuwataja baadhi ya viongozi wa kaunti, baada ya kuelezea imani aliyo nayo kuhusu mfumo wa ugatuzi, suala lililompiga chenga.
Jaji Mbogholi aidha alitakiwa kuelekeza sababu za kutojiunga na mitandao ya jamii kama vile facebook na twitter, ambayo hutumiwa na wengi enzi ya sasa. Jaji huyo ameahidi kuifanyia mageuzi makuu idara ya mahakama, kukiwamo kurejesha ofisi ya Msimamizi Mkuu wa Mahakama atakayekuwa na jukumu la kuhakikisha majaji na mahakimu wanakamilisha kesi zilizowasilishwa mbele yao kwa wakati. Wakati uo huo, ameahidi kuwapa haki ya kusikilizwa majaji ambao watakata rufaa baada ya kuachishwa kazi kupitia mchujo ulioendelezwa na kamati ya Sharad Rao.
Jaji Mbogholi amekuwa wa pili kuhojiwa baada ya jaji Alnashir Visram. Jumatano itakuwa zamu ya Jaji David Maraga.
 

Premium Article

Get Full Access for Ksh299/Week.

Fact-first reporting that puts you at the heart of the newsroom. Subscribe for full access.
Continue Reading  →
What you get
  • Unlimited access to all premium content
  • Ad-free browsing experience
  • Mobile-optimised reading
  • Weekly newsletters & digests
Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payments Kenya's most trusted newsroom since 1902
Support Independent Journalism

Stand With Bold Journalism.
Stand With The Standard.

Journalism can't be free because the truth demands investment. At The Standard, we invest time, courage and skills to bring you accurate, factual and impactful stories. Subscribe today and stand with us in the pursuit of credible journalism.

Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payment Kenya's most trusted newsroom since 1902