Jiji la Nairobi leo hii liliamkia tukio la shambulizi la bomu ambalo lilifanyika katika baa moja inayotambulika kama Mwaura ambayo ipo kwenye barabara ya Mfangano hapa jijini nairobi . Mlipuko huo unasemekana kusababishwa na gurenedi lililotupwa ndani na baa hiyo na kusababisha kujeruhiwa kwa watu 12. Hata hivyo haijabainika aliyesababisha mlipuko huo. Mwanahabari wetu Saida Swaleh ana mengi zaidi.