Mashahidi Wazungunuza

Hatimaye mbunge wa Eldoret kaskazini William Ruto amewasilisha rasmi malalamishi dhidi ya tume ya kitaifa ya kutetea haki za binadamu anayodai iliwahonga mashahidi ili kutoa taarifa potofu kumhusu. mapema hii leo jamaa wawili, Ken Barzizi wekesa na William Kipkemboi rono walijitokeza na kudai kwamba walilipwa na tume hiyo ya kitaifa ya haki za binadamu ili kutoa ushahidi potofu unaomlenga William Ruto. lakini licha ya kuzungumza na waandishi habari katika nyumba walimokuwa wanaishi huko kilimani,taarifa zao zilionekana kukanganyana.