Chaguzi ndogo zitakazofanyika tarehe 27 mwezi huu zinatarajiwa kuwa mchuano wa kihistoria kwa Rais William Ruto, akiwa katika harakati za kuhakikisha ana nafasi bora ya muhula wa pili mwaka 2027.
Ushindi au kushindwa katika eneobunge la Malava utaibua maswali makubwa kuhusu mustakabali wa kisiasa wa serikali ya Kenya Kwanza, hususan iwapo itabidi kuwepo na mabadiliko ya uongozi au kuendelea na usanifu wa sasa unaowapa nafasi viongozi wa Magharibi, Musalia Mudavadi na Moses Wetang’ula.