Serikali ya Kenya Kwanza inaendeshwa kwa njia ya magendo, amesema Kiongozi wa Azimio, Raila Odinga.
Akihutubu katika mkutano wa wananchi kwenye Kaunti ya Muranga, Odinga amedai kwamba serikali inatumia watu fulani kuagiza mahindi kutoka mataifa mengine ili kujipatia faida, gharama ya maisha ikisalia juu.