.
27th January, 2022
Viongozi wa muungano wa One Kenya kwa mara nyingine tena wamewashutumu Musalia Mudavadi na Moses Wetangula kutokana na kile wamesema kuwa ni usaliti baada ya wao kuhama muungano huo na kujiunga na Naibu Rais William Ruto.
Akizungumza katika mikutano ya hadhara katika kaunti ya Kitui kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka na mwenyekiti wa Kanu Gideon Moi wamesema kuwa Mudavadi na Wetangula walishindwa kustahimili mawimbi ya kisiasa na hivyo kuamua kutoroka.