16th January, 2021
kwa mara nyingine kinara wa odm raila odinga amesisitiza kuwa hakuna kurudi nyuma kwa suala la kura ya maoni na kuwa hakuna atakayesimamisha azimio la kuleta mabadiliko ya kikatiba nchini. odinga aliyefanya kikao na kina mama wakiongozwa na viongozi kina mama siku moja baada ya kukutana na vijana wa hapa jijini nairobi amesema kuwa wana mipango kupigia debe bbi hadi mashinani. msimamo huu umeshikilia na viongozi mbali mbali wa kisiasa kama anavyoarifu sasa daniel kariuki