21st October, 2020
Siku moja tu baada ya Shabana kuilaza Afc Leopards bao moja bila jibu na kutwaa taji la mashujaa, Rais Uhuru Kenyatta ameikabithi timu hiyo basi lenye uwezo wa kubeba abiria 62. Akizungmza kwenye hafla ya kupeana basi hilo, Rais Kenyatta ameitaka Shabana kukaza buti, kuimarisha viwango vyao ili kurejea ligi kuu ya kitaifa KPL.