.
1st June, 2020
Rais Uhuru Kenyatta ameashiria uwezekano wa kufanywa kura ya maamuzi kabla ya uchaguzi mkuu wa 2022. Kwenye hotuba yake kwa taifa wakati wa maadhimsho ya sikukuu ya Madaraka, Rais alisema katiba iliyoko sasa inastahili kufanyiwa marekebisho ili kuendeleza demokrasia na kujumuisha jamii zote katika uongozi wa serikali ili kuzima ghasia za baada ya uchaguzi.