.
1st June, 2020
Mafuriko yamewatatiza wenyeji wa kaunti ya Lamu baada ya mito kuvunja kingo kutoka kaunti jirani ya Tana River. Wenyeji sasa wameachwa bila makao kwani nyumba zao zimezama kwenye gharika. Kwa sasa wanategemea msaada kutoka serikali kuu pamoja na shirika la msalaba mwekundu ili kujimudu kimaisha.