.
1st June, 2020
Jamaa mmoja katika kijiji cha Oldonyo Kajiado ya Kati amenusurika kifo baada ya kushambuliwa na simba ambao wanahangaisha kijiji hicho. Wafugaji wanakadiria hasara kubwa kufuatia uvamizi wa simba hao ambapo zaidi ya ngombe 40, mbuzi na punda wameuawa huku mifugo wengine wakiachwa na majeraha. Wafugaji wanadai kwamba uvamizi huo unaendelezwa na simba watatu na hii leo waliungana ili kuwatafuta simba hao. Wafugaji hao wamekashifu shirika la huduma kwa wanyama pori nchini kwa kuzembea kwenye kazi yao wakisema hii si mara ya kwanza simba kuvamia mifugo katika eneo hilo na hakuna hatua inayochukuliwa.