.
28th May, 2020
Wabunge wa mrengo wa NASA wamefanya kikao cha bunge ambapo waliamua kwa kauli moja kuwatimua wabunge tisa kutoka kamati za bunge. Mbunge wa Kiminini Chrisantus Wamalwa ametimuliwa kama naibu kiranja wa wachache katika bunge la taifa na mahala pake kuchukuliwa na Mbunge wa Tongaren David Eseli Simiyu.
Mbunge wa Malindi Aisha Jumwa ametimuliwa kama kamishna kwenye tume inayosimamia masuala ya bunge na ikapendekezwa nafasi hiyo ichukuliwe na mbunge wa Likoni, Mishi Mboko. Kiongozi wa wachache katika bunge la taifa, John Mbadi amesema utaratibu wa kumtimua Aisha Jumwa kirasmi umeanza.