.
21st May, 2020
Serikali imetakiwa kuimarisha mpango wa kugawa chakula kwa familia zilizopoteza ajira kutokana na janga la Korona.
Akizingumza alipoongoza shughuli ya kutoa msaada wa chakula na vifaa vingine vya matumizi kwa familia masikini mtaani Kayole, Askofu Geoffrey Migwi, wa House of Hope Church, alisema familia nyingi zinahitaji kusaidiwa kwenye majira haya magumu ya homa ya Korona.
Aidha aliwarai wanasiasa kuonesha mfano mwema kwa kuwajali wasiojiweza badala ya kupiga siasa tu.