.
14th May, 2020
Hatubabaishwi wala kutikiswa na vitisho ndo ujumbe wa kundi la Inua Mama la mrengo wa Tanga Tanga katika chama cha Jubilee, ujumbe waliomsukumia kiongozi wa chama rais Uhuru Kenyatta na msemaji wake Raphael Tuju.
Mbunge wa Kandara Alice Wahome pia amekejeli tishio kwamba, chama tawala kitaanzisha mikakati ya kuwapokonya viti wabunge waliochagulia na kusema kwamba hiyo ni ndoto ya saa sita mchana.