9th March, 2020
Polisi mjini busia kwa ushirikiano na wenzao wa nchi ya jirani ya uganda wamefanikiwa kunasa bunduki aina ya ak 47 na risasi 25 iliyokuwa imefichwa kwenye paa ya nyumba moja ya kukodi katika mtaa wa bondeni mjini Busia. Kamanda wa polisi kaunti ya Busia John Nyoike amesema bunduki hiyo inakisiwa kuibwa kutoka kwa polisi wa uganda miezi kadhaa iliyopita kabla ya kuanza kutumiwa na mshukiwa akiwa na wahalifu wengine kutekeleza visa vya uhalifu na mauaji katika maeneo ya Busia Kenya na Uganda.