8th March, 2020
Mzazi wa kike kutoka jamii ya wafugaji amelaumiwa kwa kuwa chanzo cha mila potovu ya ukeketaji miongoni mwa wanao wa kike. Hili limejitokeza kwenye warsha ya kuadhimisha siku ya wanawake ulimwenguni ambapo mashirika mbali mbali ya jamii yamewataka wazazi wa kike kusimama kidete katika vita dhidi ya mila hiyo ambayo inamnyima fursa mtoto wa kike kupata masomo.