17th February, 2020
Zaidi ya wanafunzi 300 wa kike waliojifungua kabla ya kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu katika kaunti ya kakamega wamepokea msaada wa karo, mavazi, maziwa ya watoto wao pamoja na vyakula. Wanafunzi hao wanasoma katika shule mbalimbali katika kaunti hiyo. Watoto wao wachanga pia walizawadiwa bidhaa mbali mbali za kukimu mahitaji yao katika hafla iliyoongozwa na mwakilishi wa kike elsy muhanda. Wanafunzi hao walielezea furaha yao kuwa jamii haijawatenga na msaada wanaopata umewapa motisha ya kuendelea na masomo