.
27th January, 2020
  Wakazi wa mji wa Garissa wamefanya maandamano ya amani kuishinikiza serikali kuimarisha usalama katika eneo hilo ili kuzuia mashambulizi ya mara kwa mara kutoka kundi la wanamgambo wa alshabaab kutoka Somalia. Wakizungumza baada ya maandamano hayo, wanaharakati kutoka kaunti ya Garissa wakiongozwa na Mwalimu Salah Yusuf wamelaani shambulizi la hivi maajuzi lililowalenga wanafunzi pamoja na walimu.