27th January, 2020
Balozi wa marekani ameshauri kwamba ingekuwa fahari ya serikali ya marekani ikiwa wanasiasa hawataanza kuingiza siasa kwenye mikutano ya ripoti ya upatanisho, BBI. Balozi kyle mccarter ameyasema hayo alipokuwa huko bungoma kwa ziara rasmi, ambapo amewataka wakenya kuiichukulia kwa uzito ripoti hiyo na kuijadili kwa misingi ya maudhui yaliyonuiwa kamati hiyo ilipoundwa Katika ziara ya kujifahamisha na miradi ya eneo hilo,alipokelewa na mwenyeji wake, gavana wa Bungoma, Wycliffe Wangamati.